04 Kristo na Ibada Binafsi; Kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli Inamaana gani? (Nyayo za Kristo)

25 Januari, 2025

Kitabu: Yohana

Bible Passage: Zab 25:14, Yoh 4:23

Katika masaa 24 ambayo Mungu anatupa kila siku. Je! tunatenga muda wa kumwabudu Mungu wetu? Ungana na Ndugu Mikael kujifunza zaidi kuhusu umuhimu wa kuwa na uhusiano na Yesu. Katika Yoh 4:23 Neno la Mungu linasema; “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.” Inamaana gani kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli? Yesu alisema: “Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.” (Yohana 15:14) Tunapaswa kufanya nini hasa ili tuwe karibu na Mungu? Karibu katika somo hili ili uelewe zaidi mambo hayo. Mungu akubariki.

Mafundisho haya yanaendana na masomo yanayopatikana katika Kozi ya Maji ya Uzima inayoitwa Nyayo za Kristo. Kwa maelezo zaidi kuhusiana na masomo haya au kujiunga na kozi wasiliana nasi kupitia

Barua pepe: neno@majiyauzima.com

Simu: +255754 490 549 / +255694 298 395 / +255719 275 767