05 Kristo na Mawazo; Je! Mungu Anajali Kuhusu Mawazo Yetu? (Nyayo za Kristo)

31 Januari, 2025

Kitabu: 2 Korintho

Bible Passage: 2 Kor 10:5, Fil 4:8

Neno la Mungu linasema; Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya heshima, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo. (Wafilipi 4:8)

Tunawezaje kuwa na mawazo ya namna hii? Ungana na Kaka Smith kujifunza hatua zinazoweza kutumika katika kudumisha mawazo safi. Kwa nini mawazo yetu yanakuwa na umuhimu mbele za Mungu? Matendo yetu yanaanza wapi? Mungu akubariki unapomwomba kutakasa fikra zako.

Mafundisho haya yanaendana na masomo yanayopatikana katika Kozi ya Maji ya Uzima inayoitwa Nyayo za Kristo. Kwa maelezo zaidi kuhusiana na masomo haya au kujiunga na kozi wasiliana nasi kupitia

Barua pepe: neno@majiyauzima.com

Simu: +255754 490 549 / +255694 298 395 / +255719 275 767